Anapoishi Gigy Maney Mmmh....... Hatare Tupu Utamuonea Hadi Huruma | Mara Paah

Anapoishi Gigy Maney Mmmh....... Hatare Tupu Utamuonea Hadi Huruma


LICHA ya hivi karibuni kujinadi kuwa ametupia wigi la bei mbaya alilodai kulinunua kwa shilingi milioni sita, msanii wa Bongo Fleva anayefanya poa na ngoma yake ya Nampa Papa, Gift Stanford ‘Gigy Money’ anadaiwa kuishi kwenye nyumba ambayo haina hadhi ya hilo wigi hivyo kuibua miguno.

Kufuatia madai hayo, gazeti hili lilifika kwenye nyumba hiyo anayoishi Gigy maeneo ya Sinza-Kwaremi jijini Dar na kushuhudia inavyoonekana kwa nje kuwa haina hadhi, lakini kwa ndani ni bonge la nyumba.

Chanzo makini kilieleza kwamba, mwanadada huyo anaishi maeneo hayo kwenye nyumba hiyo yenye muonekano kama banda ambapo siyo hadhi yake, hali inayowashangaza wengi kutokana na umachachari wake hivyo kujiuliza inakuwaje ashindwe kuishi kwenye mjengo wenye hadhi yake.

“Yaani Gigy anaishi kwenye banda maana muonekano wa nyumba anayoishi kwa kweli unashangaza na hapa mtaani watu wamekuwa wakimsema sana na kumshangaa kwamba inakuwaje aishi hivyo wakati ni staa mkubwa ambaye anafanya shoo na kupata fedha?” 
kilihoji chanzo hicho.

Bonyeza Picha Hapo chini Kudownload App Ya Usiku wa Mahaba Uweze Kujiunga na Magroup ya WhatsApp Ya KIkubwa Utasoma Simulizi Tamu na Kujifunza Jinsi ya Kumridhisha Mpenzi wako Bonyeza Picha Chini au HAPA

gigy-money-1

0 Response to "Anapoishi Gigy Maney Mmmh....... Hatare Tupu Utamuonea Hadi Huruma"

Post a Comment